{"product_id":"kasankala-ladislaus-usindikaji-na-matumizi-ya-unga-bora-wa-mhogo-9786200453648","title":"USINDIKAJI NA MATUMIZI YA UNGA BORA WA MHOGO","description":"Mhogo ni moja ya mazao ya jamii ya mizizi ambao ni muhimu kwa chakula na biashara hapa nchini. Mhogo una nishati lishe kwa wingi, makapi lishe kwa wingi amboyo ni mhimu kwa mmengenyo wa chakula. Muhogo ni chanzo kizuri cha vitamini C, ribofravini, niasini ambayo ni mhimu kwa mahitaji ya mwili.Kitabu hiki kina lengo la kuelimisha wakulima, wasindikaji na jamii kwa ujumla kuhusu namna bora ya kuvuna, kuhifadhi mhogo mbichi, kusindika, kuondoa sumu ya sianidi kwenye mhogo, ufungashaji na matumizi mbali mbali ya unga bora wa mhogo. Taarifa za kitalaam kuhusu uzalishaji wa unga bora wa mhogo zimeelezewa kwa utaratibu ambao ni rahisi zaidi na wa kueleweka kwa msomaji. Jambo kuu linalozingatiwa katika kitabu hiki ni uwasilishaji wa mtiririko wa uzalishaji wa unga bora unaotokana na mhogo mtamu na mchungu ambao unamrahisishia mjasiriamali msindikaji kuzalisha bidhaa bora na salama kwa mlaji.Ingawa kimsingi kitabu hiki kimekusudiwa kwa wajasiriamali na wakulima wanaohusika katika usindikaji wa bidhaa za mhogo, maelezo na miongozo iliyoainishwa inaweza kutumiwa hata na wafanyakazi wa ugani na jamii kwa ujumla ubora zinazohitajika ili kuongeza kukubalika kwa bidhaa za mhogo kwa watumiaji.","brand":"GlobeEdit","offers":[{"title":"Default Title","offer_id":53754953564502,"sku":null,"price":0.0,"currency_code":"EUR","in_stock":false}],"url":"https:\/\/www.momoxbooks.com\/products\/kasankala-ladislaus-usindikaji-na-matumizi-ya-unga-bora-wa-mhogo-9786200453648","provider":"momoxbooks","version":"1.0","type":"link"}